Mpira ulioundwa na kuambwa kwa ngozi ya mnyama uligaragazwa katika uwanja wa Wembley hapo jana. Wana wa profesa Arsen Venga walitaka kulipiza kisasi cha maboa matano kwa matatu waliyo chabangwa na mabigwa wa uingera Manchester City.
Ingawa hawakueza kulipiza kisasi hapo jana walipokuwa wakigaragaza mpira wa wavu kuwania ngao yani(community shield) jinsi inavyo ng'amuliwa na wanaokijua kimombo.
Wana wa Arsenali waliwachabanga na kuwarindima mabingwa hao wa uingereza mabao matatu bila jawabu.
Ilikuwa ni furaha kwa mashabiki wa Arsenali na pia kwa nahodha mpya Arteta baada ya kuchukua tuzo ya kwanza kwa siku ya kwanza akiwa nahadha kwa finali ya kwanza.
Msafiri ni aliye bandarini, hivi ndivo wazee wa miaka na mikaka walivyotuelimisha. Arsenali wameanza safari yao ya kuwania mataji na wamedhibitisha kwamba wanaweza kuleta upinzani mkali mashindanoni msimu huu. Langu ni kutia amcho masikio nakutaka kujibuwa na kudhibitisha msemo huu.
 |
| Arsenal players with community shield trophy |